Thursday, December 18, 2008

TUTAKUKUMBUKA DAIMA "ODONG ODWAR"

Saalam Wadau,

Ninapolitaja jina la huyo mtu hapo juu ninaamini si geni kwa wanafunzi wengi wa vyuo vikuu na Tanzania kwa ujumla.........!!
Enzi za uwepo wake alikuwa ni mwanafunzi wa sheria katika chuo kikuu cha Dar Es Saalam...na kabla ya kutimuliwa kurudi kwao Uganda alikuwa mwaka wa tatu.............!!

Tutamkumbuka huyu mpiganaji kwa mambo mengi sana...ikiwa ni pamoja na zengwe alizofanyiwa kipindi alichotaka kuwa Rais wa Daruso lakini Serikali na Chuo wakaogopa kwa kudhani kuwa UDSM patachafuka sana kwa migomo na dhambi zao zitatajwa kwa majina.................!!

Pia alikuwa mstari wa mbele katika kuongoza harakati mbalimbali pale mlimani zikiwepo harakati feki na zisizo feki...mfano halisi ni zile harakati za kuifuta 40% ambazo kiasi fulani tulifanikiwa na nyingine ndogondogo lakini kubwa zaidi ni hizi harakati feki za juzi ambazo aliziongoza yeye na ndugu zake kina OWAWA na SILINDE ambazo zilifanya vyuo vya umma vifungwe na wao wapate mabalaa na wengine kwenda kujificha mikoani.

Sitasahau jinsi tulivyimpigania kipindi alichofukuzwa chuo kwa hila kisa tu aligombea Urais na tukagoma mpaka akarudishwa yeye na wenzake na tukamuondoa rais mamluki bwana Pasience........!!

Kwanza namsifia kwa baadhi ya mambo aliyofanya he was a real HERO na kwa mambo mengine machache hayo sitaacha kumponda!!.Lakini intention ya huyu mganda ilikuwa ni nini?..bado ninajiuliza sana!!..na kwa nini alijiingiza katika vyama vya siasa vya nchini wakati yeye si raia??..bado najiuliza sana........!!

NENDA ODONG ODWAR TUTAKUKUMBUKA DAIMA....YOUR FOOTPRINTS ARE STILL THERE AT THE HILL!!

WASALIMIE MARAFIKI WA UGANDA....GOD BLESS YOU IN YOUR FUTURE ENDEVORS!!

2 comments:

Anonymous said...

hamna lolote nitalomkumbka huyu jamaa...kwa upande wangu mimi naona alituchafulia tu mazingira ya chuo na vyuo vyote....ngoja aende kwao akajifunze
na nyie wanaharakati feki mliobaki kama SILINDE,OWAWA na wengineo..jiangalienia sana..piganeni muokoe familia zenu kwa kusoma sana..huu ni ulimwengu wa kibepari na sio wa kiujamaa kwa iyo mnapoteza muda..piganieni haki zenu na za familia zenu wal sie hatukuwaalika..na hao CHADEMA wanaowatumia wanawapotezea muda,na nyie washenzi wa CCM ndo mnasababisha yote haya yatokee..jirekebisheni
SHWWWWWAAAAAAAAAAIIIIIINNNNNNN!!

Anonymous said...

kukubali kuburuzwa kuna mambo!?

watanzania tuna ifiriority mtu akitoka nje ya nchi yeyote tunamuona yuko juu kuliko sisi na kumpa nafasi ya kutuendesha,

hii ipo mpaka kwa viongozi wetu ambao wanapendelea zaidikuwaajiri wageni ijapokuwa hana sifa eti ni mgeni,wakati raia hawana ajira,

acha watuibie,uchumi hawendi mbele na fisadi hazishi,

hakuna mtu mwengine yeyote mwenye uchungu na tanzania zaidi ya watz wenyewe

kazi kwenu!