Tuesday, December 30, 2008

BONOFACE ELPHACE MAGINA,WE SALUTE YOU!!

My stakeholders, Can you accompany me in paying a tribute to the boy named above, Let us acknoweldge his utmost contribution for the betterment of Tanzanians Studying in Russia.....!!

Ni mnamo wiki iliyopita ubalozi wa TZ nchini Urusi umemfukuza nchini humo mwanafunzi huyu na kumrudisha nyumbani TZ.Alikuwa ni Rais wa wanafunzi wa Kitanzaniua wanaosoma Chuo Kikuu Cha Urafiki Lumumba jijini Moscow.

Kisa cha Kumfukuza ni nini??
Kwa sababu ya kufuatilia kwa nguvu zote fedha za wanafunzi wa kitanzania wanazotumiwa na serikali ambazo inasemekana zinaliwa na Ubalozi huo badala ya kuwafikishia wanafunzi!!

Kwa hiyo ubalozi ukaamua kumfukuza na kumkatisha masomo........Serikali mnafanya nini??Pliiiiiz jaribuni kuwa na aibu na kushughulikia swala hilo mwenzetu arudi Chuoni......!!
Huyu ni mpiganaji wa ukweli na mwanaharakati wa Ukweli,Alitrafuta haki ya wenzake peacefully huko Ughaibuni!!

BONIFACE ELPHACE MAGINA WE SALUTE YOU...VIVA OUR TRUE HERO!!

SALAMU KUTOKA KWA MDAU WA DELHI..INDIA.



nawatakia wadau wote wa blog yako x-mass njema na mwaka mpaya.nadhani huu ndio muda wa kujifanyia tathmini wapi tulikotoka na wapi tunaenda,yepi tumefanikiwa na yepi hatukufanikiwa na kuweka strategic intent sawa pae kwenye makosa.


mdau miki kilima from university of delhi,

newdelhi,

india


miki kilima

master of commerce(finance)

department of commerce

delhi school of economics

university f delhi

KWA NINI UDOSO MNAJITENGA NA WENZENU???

UDOSO KUTOJIUNGA NA 'UVEJUTA' NI KOSA KUBWA SANA
Serikali ya wanafunzi wa chuo Kikuu cha Dodoma (UDOSO) imeendeleakufanya madudu mengine kwa kutojiunga na Umoja wa Vyuo vikuu naTaasisi za Elimu ya juu vya Umma Tanzania (UVEJUTA).Alipoulizwa hivikaribuni,Rais wa UDOSO Bw.Joramu Malimia lidai eti kutokushirikishwakatika uanzishwaji wa Umoja huo.Hoja hiyo haina msingi kabisakiuhalisia.
Umoja huo ambao hivi sasa unaundwa na vyuo na taasisimbalimbali za Umma kama vile Chuo Kikuu cha Dar s salaam (UDSM),Chuokikuu kishiriki cha Elimu Dar es salaam (DUCE),Chuo Kikuu kishirikicha Elimu Mkwawa (MUCE,Taasisi ya teknolojia ya Dar Es salla (DIT) navingine umeendesha mgomo wa kupinga Sera mbovu ya Serikali yaUchangiaji wa Elimu ya juu,Ongezeko la Ada pamoja na mambo menginemengi ambayo kimsingi hayaendi vizuri.Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) ni Chuo cha Umma,hivyo haikuwa na sibusara kwa uongozi wa UDOSO unaoongozwa na Bw.Malimi kutojiunga naumoja huo.

Viongozi wa UDOSO wanapaswa kujua kwamba kujiunga na Umojahuo si Lazima kushiriki katika kila maamuzi yao ambayo wenyewe wataonahayana msingi.Kwa madai wanayogomea wenzetu hao,ni ya Msingi kabisakwani sisi watoto wa masikini ndio tuanoumia na sera hizi mbovu zaSerikali za uchangiaji wa elimu ya juu.Nina uhakika mkubwa kwamba viongozi wa UDOSO hawakubaliani kabisa nasera mbovu ya uchangiaji wa Elimu ya juu,kama vile Madaraja ya utoajimikopo yasiojali hali za watu,ongezeko kubwa la ada,madaraja ya pesaya Vitendo na mengine mengi.Sasa hiyo hoja ya kutaka mpakamshirikishwe,sijui muandikiwe barua sidhani kama ilikuwa na umuhimuwowote.Kwa kuwa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) ni Chuo chaumma,Bw.Malimi na Viongozi wenzie wa UDOSO wakae na watafakari kwakina Umuhimu wa kujiunga na Umoja huo wa Vyuo vikuu vya Umma.Hii nikwa sababu wanaweza kujiunga halafu wakakataa kushiriki katika Mgomohuo unaoendelea kuliko kutojiunga na kutoshiriki katika mgomo huowakati chuo Kikuu cha Dodoma ni Chuo cha Umma na sababu za Mgomo huoni za Msingi kabisa.

Chondechonde UDOSO harakisheni Kujiunga na UmojaHuo mpya wa vyuo vikuu vya Umma (UVEJUTA) ili nasi tuunge nguvu zetudhidi ya Matatizo yanayowakabili Wanafunzi wa vyuo Vikuu vya Ummanchini.

SELEMANI TAMBWE
BA. PSPA
Chuo Kikuu cha Dodoma

HAPPY HOLIDAYS SEASON TOKA KWA MAKULILO Jr,



MAKULILO Jr,

makulilo@marshall.edu
Ndugu wadau,
Napenda kutoa salamu za kipindi hiki cha siku kuu (Holiday Seasons), Heri ya Siku kuu ya Noeli na Mwaka Mpya 2009. Blog ya SCHOLARSHIPS
www.makulilo.blogspot.com inashukuru kwa ushirikiano wa wadau wote hadi kufikia hatua hii (sasa ina miezi 7). Blog inaahidi mambo mengi mazuri, na inatoa wito kwa wadau kufanya applications zaidi khs masuala yetu ya NONDOZI KWA WADAUZI.

Note: Nimeambatanisha na picha yangu, hapo nilikua vekesheni nje ya mjengo wa kaka Barry Obama (WhiteHouse) Washington DC.

MERRY CHRISTMASS & HAPPY NEW YEAR 2009


scholarships101@aol.com
+1 304 633 0978

Wednesday, December 24, 2008

VYUOTZ TEAM TUNASEMA HIVI.........!!

Nimewahi kusikia msemo wa kiingereza unaosema kuwa "good people are good because they ave come to wisdom through failure,we get very little wisdom from success" kwa kiswahili ukimaanisha kuwa watu wema ni wema kwa sababu wamepata hekima kupitia kushindwa kwao,tunapata hekima kidogo sana kupitia mafanikio.

Moja kwa moja ninaekwenda kwenye kusudio la waraka huu kwenu wadau wa vyuotz blogu.kutokana na athari kubwa tulizozipata wanafunzi wa vyuo vikuu na kushindwa kukubwa kwa migomo iliyoandaliwa na viongozi wa wanafunzi na wale wajiitao wanaharakati tumeamua kuungana na kupinga na njia kama hiyo kama utatuzi wa matatizo ya wanafunzi wa vyuo vikuu.

Hebu angalia habari hiyo hapo chini ya gazeti la mwananchi,hizo ni athariwalizozipata dada zetu na wanafunzi wengi wa mikoani walipata shida sana siku wamefukuzwa chuo,na bado athari nyingine nyingi zitaonekana kama zakupoteza muda wetu,kuharibu ratiba za mafunzo kwa vitendo kwa mwaka ujao,chuo kuingia hasara,wanafunzi wa nchi za nje kurudi kwao bila hata semista kuisha na wengine kubaki chuo bila kufanya lolote sababu wenzao hawapo.Kubwa ni dada zetu ambao hata hawakugoma wapo wanauchuma ukimwi kutoka kwa watu ambao siku hizihujulikana kama mafataki!!

Nadhani sasa wanafunzi wengi sasa watakuwa watu wema na watakuwa na maamuzi ya hekima kutokanana kufeli na kushindwa kwa migomo yao,sababu sera hiyohiyowaliyoikataa ndio wamejaza fomu kuikubali,sasa kwanini tuligoma??

Kutokana na kupoteza muda wetu sana,kuharibu ratiba zetu sanana kuharibu malengo yetu sana kutokana na migomo ambayo wanafunzi wengi hawajui siri yake, kwanimingi imeandaliwa na wanasiasa wa vyama fulani na kuwasponse wanafunzi fulani ili waiongoze migomo hiyo na pia kuwaconvice baadhi yaviongozi wa wanafunzi iliwapitishe migomo.....Tulipata kumsikia kiongozi mmoja wa chama cha siasa akisema"Lazima tuwachafue sana chama fulani(jina kapuni)mwaka huu"....alikuwa akiongea wakati wanapanga mgomo huu uliopita....Na siku kabla ya mgomo tukamsikia mwanafunzi mmoja ajiitaye mwanaharakati akimpigia simu kiogozi wa siasa akimwambia "dont worry tommorow you will seeon the media....iliwauma sana wanafunzi wasiopenda migomo.....!!kwani aliisema kauli hiyo akiwa Bar ya maeneo yaleyale ya chuo

Hapa sasa inaonyesha kuwa vyama vya siasa vinatumia vyuo kama "battle ground" yao,hasara tunapata sisi lakini hivyo vyama vya siasa vinaendelea kudumu..tunaingiziwa siasa vyuoni hasara twapata sisi wenyewe kwani wanaharakati hao wamejificha sehemu flaniflani wakiendelea kula mipesa kutoka kwenye vyama vyao.na madai yao wakitimuliwa chuo wanaandaa mgomo wa kuwarudisha!!tunalipinga hilo wana vyuotz......!!
Sasa kama team ya vyuotz na baadhi ya wanafunzi tuliokaa kikao na kutathmini swala hili na athari yake kwa watu wengi na familia za wanafunzi na taifa kwa ujumla tunasema hivi.

(a) Tutaendelea kuzisema athari za migomo na kuwaelimisha wanafunzi watafute njia nyingine za suluhisho la matatizo badala ya migomo.......Na viongozi wa wanafunzi na wanaharakati vyuoni wasiwapotezee muda wanafunzi kwa maslahi yao binafsi na vijihela wanavyopata wakati wanafunzi wengi wanapata shida,dada zetu wameweka rehani miili yao ili waishi mjini na wapate ada za kulipia warudi chuo na wengine wako vijijini wanahangaishana na wazazi kupata hayo malaki ili warudi vyuoni.Lakini wanasiasa walioiandaa tunawaona kila siku mjini kwenye magari yao na hawatusaidii lolote....!!.....Hivyo tunawaomba wadau muisapoti blog yetu iendelee ili tuadress hili tatizo na mengineyo,angalia hapo juu kulia palipoandikwa VOLUNTARY CONTRIBUTION ili ushiriki nasi.

(b) Pili tumeamua kuunda Chama kitakacho adress hilo tatizo la fujo na migomo na tutakisajili kioperate vyuo vyote TZ paler tutakapopata sapotio.Wanafunzi 12 wa vyuo mbalimbali wameonyesha nia na kukaa kikao juzi.majina yao tunayo na ntawapa soon.Profile ya Chamahicho nikamaifuatavyo

Name ofAssociation: Humble Students Against Strikes &Boycots(HSASB)

Motto: There is an alternative best solution instead of strikes and boycotts

Aim: Adressing the effects of boycots & strikes

Mission:To liberate the minds of students so that theycan find other proper means of acquiring their rights.

Vission: Having the secure environment at our Campuses for Study and Life.

Tafakarini Wadau na Chukueni hatua,kama upo tayari kuisapoti nia yetu tunaomba uisapoti blog yetu kuichangia ipate facilities iendelee kuwepo na karibuni watu au mashirika aumawakala mlio tayari mkusapoti chama hicho kiwepo!!Kama uko tayari kusapoti blog fanya hivo Voluntary Contribution kwenye Bank A/c na Kama uko tayari kusapoti Hicho chama tutumie Email Kwenye billjax.nyakua@gmail.com
Vyuotz Team.


Tuesday, December 23, 2008

KWELI ATHARI ZA MIGOMO NI KUBWA....!!

Kutoka gazeti la Mwananchi la leo.

MARA baada ya kutolewa kwa amri ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kusimamishwa masomo na kutakiwa kuondoka chuoni mara moja, mambo mawili makuu yaliumiza vichwa vya wanafunzi walio wengi. Mosi watakwenda wapi na pili wataishi vipi ndani ya muda wote chuo kikiwa kimefungwa.Kwa wakazi wa Dar es Salaam, mikoa ya jirani na hata wale wenye jamaa wa karibu mambo haya hayakuwasumbua kwa kuwa walijua nini cha kufanya. Kibarua kilikuwa kwa wale wanaotoka mikoa ya mbali na wakawa hawana kitu mfukoni.Ni mwezi mmoja na ushee sasa tangu kufungwa kwa chuo hicho uchunguzi wa Mwananchi umebaini kuwa baadhi ya wanafunzi wa chuo hicho wameamua kujiingiza katika biashara ya ukahaba kwa kile wanachodai kupambana na ugumu wa maisha unaowakabili baada ya kukosa njia za kurudi makwao.Safari ya gazeti hili kutaka kujua ukweli wa tetesi kuwa baadhi ya wanafunzi waliofukuzwa wanajiuza mitaani zilianzia hosteli ya Mabibo.

Dada mmoja (jina tunalihifadhi) alikuja pale kuomba hifadhi kwa wenzake wanaosoma Taasisi ya Mawasiliano ya Umma na Uandishi wa Habari (IJMC) ambao wao walikataa kugoma.Akizungumza huku akibubujikwa na machozi alisema alikwenda kuwaomba wampe hifadhi baada ya kuchoka na manyanyaso nyumbani kwa mjomba wake aliyekuwa akiishi kwake tangu chuo kilipofungwa. Anamtaja mke wa mjomba wake kama sababu ya kuchukua uamuzi wa kuhama kwa mjomba wake ambaye alikuwa safarini.Huu ndio uliokuwa mwanzo wa kujua kama yapo mambo mengine yanayowasibu wanafunzi wa chuo hiki kikongwe nchini.Nilipomsaili hakusita kusema kuwa kufungwa kwa chuo kumesababisha wanafunzi wengi wa kike kufanya biashara ya kuuza miili yao maeneo mbalimbali ya jiji hasa kumbi za sterehe na burudani."Hamuwezi kuamini nendeni hata hizi baa zilizopo hapa jirani na hosteli utawakuta wanafunzi kama hamuwafahamu mimi nitawaonesha wanajiuza, wanavaa mavazi ya kubana wana weza kununua bia moja au soda kuanzia mchana mpaka jioni wakiwa wanasubiri wanaume, na sio hapa tu hata kule maeneo ya Sinza , makumbusho na Mwenge, kwa kweli hali inatisha sana nyie wenzangu msicheke" alisema kuwaambia wenzake huku akisikitika.Ushabiki wangu wa kutaka kujua zaidi hasa nikitilia maanani hii ilikuwa kazi niliyopewa na mkuu wangu wa kazi nililazimika kumuomba dada huyu twende katika moja ya baa alizozitaja ili nikajionee fahari ya macho.Alikubali na tulijongea baaz ya jirani ambalo naomba kuhifadhi jina lake.Pale niliwakuta akina dada kadhaa alini macho yangu yalituwama kwa mabinti wawili walikouwa wameva nguo fupi huku wakipiga simu na kutoa matusi. Nakumbuka mmoja alikuwa alimaka:‘"inakuwaje mwanume kama huyu atusumbue akili zetu kama angekuwa hana pesa si angesema tusije hapa, shoga nakuomba kuanzia leo usimtafute kama ataamua atakutafuta mwenyewe"Kuanzia hapa nikaanza kupata picha fulani ambayo punde tu ukweli wake ukaja kujidhihirisha baada ya yule dada niliyemuomba kunionyesha hao machangudoa aliponambia maneno yafuatayo:"Kaka umewaona watu wako uliokuwa unawataka ndio hao, hapa ni kidogo tu wewe ukitaka kuwaona wengi nenda Makumbusho ,Mwenge au Sinza kila baa utawakuta wanafunzi, wamesheheni wakiwa wanasubiri wateja wao kama hawa, watoto wadogo lakini ndio hivyo tena.”Baada ya kujionea ya hosteli nilimwomba tena mwenyeji wangu anipeleke eneo la Mwenge kujionea hali ilivyo huko.Hapa nilishuhudia idadi kubwa ya wanawake na magari.

Wanaume walikuja na kuwachagua wanawake kama vile mtu anavyochagua chungwa gengeni."Unamuona yule mwanafunzi yule kashachukuliwa masikini kama angeniona hapa sikui ingekuwaje, lakini ndio ameshaamua jamani yaani hata Jati (jina si rasmi) na yeye anajiuza kweli hali imekuwa mbaya"alisemaKwa kuwa ilikuwa usiku kiasi mwenyeji wangu aliamua kuondoka, nilimshukuru nami nikaamua kwenda kumalizia uchunguzi wangu Makumbusho katika baa moja maarufu eneo hilo . Niliyoyakuta huku ni sawa na ya Mwenge ila hapa kidogo nilipata ugumu kung’amua nani mwanafunzi nani si mwanafunzi. Hata hivyo niliweza kuwabaini baadhi baada ya kuwasikia wakichanganya lugha za Kiswahili na Kiingereza katika mazungumzo yao. Nilihisi walikuwa wanafunzi na ndivyo ilivyokuwa.Niliamua kumfuata mwanadada mmoja aliyekuwa ameketi peke yake, nilimsalimia na kuomba ruhusa ya kujiunga naye katika meza. Nikapata muda wa kurusha ndoano yangu ya kwanza.Sikiliza majibu yake “"Kaka ikiwa unataka kutoka na mimi leo tafadhali nihakikishie kuwa utanipatia elfu kumi kwa usiku mmoja , pia ujue chakula kitakuwa ni juu yako na vinywaji sawa?nadhani umenielewa kaka vinginevyo itakuwa ngumu kaka yangu"Kwa kuwa mimi si mkware na wala sikwenda pale kwa kile ambacho yeye alikifikiri kwa mara ya kwanza nilitaka kuzungumza naye mambo mengine ambayo kwa bahati nzuri alikubali kwa roho moja.

Mwanadada huyo aliyeonekana mdogo kiumri alianza kuniambia kuwa yupo mwaka wa tatu Chuo kikuu cha Dar es Salaam akisomea fani ya sheria, alisema hafanyi biashara hiyo kwa kupenda bali ni kutokana na maisha kuwa magumu“Usione hivi kaka hapa nilipo nipo katika wakati mgumu sana kwani najua ni aibu kufanya hivi lakini, sasa nifanyeje tunakaa chumba kimoja maeneo ya kinondoni tupo watu wanane na wale wenzangu uliowaona wamekaa hapa na kila siku tunatakiwa kula na kufua wewe unafikiria tutatoa wapi hizo pesa" alifafanua sababu ya kufanya uchangudoa.Kwa hali yoyote haya ndiyo matokeo ya kukaidi amri ya chuo na ile ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Prof. Jumanne Maghembe, iliyowataka kusitisha mgomo na kurudi madarasani wakati wizara ikishughulikia madai yao.Si wote waliogoma lakini mwisho wa siku ilibidi rungu la serikali kuwaangukia waliokuwemo na wasiokuwemo.Inasikitisha.

http://www.mwananchi.co.tz/

JAMANI JAMANI VIONGOZI WA WANAFUNZI HEBU TOENI FIKRA MBOVU VICHWANI KUWA MIGOMO NDIO SULUHISHO LA MATATIZO YETU.

Monday, December 22, 2008

MASTERS BIN NONDOOZ ULAYA MAGHARIBI....!!!

Naomba uweke tangazo hili ktk blog yetu ya jamii watu wapate NONDOZI hapo.Hizi ni Scholarships za ERASMUS MUNDUS

1. Master of Innovation Management
http://www.globalin novationmanageme nt.org/

http://www.globalinnovationmanagement.org/Application_Process.html

2. Master in Strategic Project Management
http://www.mspme.org/

3. Master of Information Technology
http://www.immit.eu/default.htm

4. European Master in Work, Organizational and Personnel Pyschology http://www.uv.es/erasmuswop/

NOTE:
Mkuu hizi zote hazina complications, zote ni za Ulaya ya magharibi, zipo chini ya Erasmus Mundus.


MAKULILO Jr

DAMU YA YOYOTE ATAKEYEPOTEZA CHUO...IWE JUU YENU VIONGOZI WA WANAFUNZI.......!!


Mlipowataka wagome ili mtimize malengo yenu enyi DARUSO na viongozi wa wanafunzi wa SUA,MUCCOBS,ARDHI,DUCE,MUCE na DIT walifanya hivyo pasipo kujua ni nani amepanga huo mgomo.....!!
Mlipowaomba waandike mabango na wakatae kuingia darasani ili malengo ya wanaharakati feki yatimie...masikini wanafunzi waliitikia wito wenu na kuwaamini.................!!
Mlipowahamasisha waimbe kwa nguvu na wakimbie kwa nguvu na wahamasisheni...masikini wanafunzi waliitikia wito wenu na kufanya hivyo...........!!
Sasa wapo vijijini kwao na wameambiwa warudi kwa mashrti kibao...na wengine watashindwa......!!
Kibaya zaidi wale wa Ushirika wameambiwa walete na vyeti vyao vya form 4 na 6 wadahiliwe upya......................!!
Endapo mwanafunzi yeyote yule atapoteza chuo kwa upumbavu wenu viongozi wa wanafunzi........basi damu yake iwe juu yenu..........!!....Laana iwe juu yenu kwasababu sasa wapo kwenye matatizo mpo kimya na hamuwasaidii chochote...ila wao waliwasaidia kutimiza malengo yenu..........!!
HEBU NENDENI KANISANI MTUBU MAKOSA YENU NA MUMUOMBE MUNGU ASIPOTEE HATA MWANAFUNZI MMOJA..SABABU LAANA ITAKUWA JUU YENU!!

WAKATI WA KUIMBA NA KUKIMBIAKIMBIA RAHA SAANA...LAKINI....!!!


Natuma salamu zangu kwa mjiitao wanaharakati popote mlipo....saalam pia kwa wote mliokuwa mnaimba kama sio juhudi zake baba wa taifa....salamu kwa wote mliokuwa mkitumia slogan yenu feki ya eti mpaka kieleweke......!!
ilikuwa raha sana kukimbikimbia around chuo....na ilikuwa raha sana kuimba na kukataa vipindi mkiwa na wenzenu pale chuoni.........!!
Ujinga wenu ni pale mlipokuwa hamjui ni nini na ni nani aliye nyuma ya mgomo wenu feki......!!!
Walewale waliokataa sera..haohao wanajaza fomu ya kuikubali sera..................!!
mama yangu....kweli mmekosa akili ya upambanuzi wa mambo............mlikuwa mnaona raha sana kuimba mkiwa pamoja..ila sasa kila mtu yuko nyumbani kwao na ndipo anapogundua kuwa kila mtu atabeba mzigo wake mwenyewe.....!!
Sasa unahangaika wewe na mama yako kutafuta fwedha ulipe urudi chuoni...........!!Ilikuwa raha sana kuimba na kutoka jasho...ila mtoto wa mwaka wa kwanza na wa pili alipoambiwa rudi nyumbani huku nauli hana mfukoni....ndipo alipokumbuka kuwa kila mtu atabeba mzigo wake mwenyewe....Niliwakuta Ubungo Bus Terminal wakiwa wamebung`aa na mimacho yao hawajui pa kwenda.....!!...Muwe na fikira zinazojitegemea na msiongozwe na hao wanaharakati feki wanaokuwa sponsored na watu fulani.....!!
HAYA ENDELEENI KUJAZA FOMU ILI MRUDISHWE....ILA MKIRUDI KAENI CHINI MUORODHESHE FAIDA NA HASARA MLIZOPATA....!!

Thursday, December 18, 2008

TUTAKUKUMBUKA DAIMA "ODONG ODWAR"

Saalam Wadau,

Ninapolitaja jina la huyo mtu hapo juu ninaamini si geni kwa wanafunzi wengi wa vyuo vikuu na Tanzania kwa ujumla.........!!
Enzi za uwepo wake alikuwa ni mwanafunzi wa sheria katika chuo kikuu cha Dar Es Saalam...na kabla ya kutimuliwa kurudi kwao Uganda alikuwa mwaka wa tatu.............!!

Tutamkumbuka huyu mpiganaji kwa mambo mengi sana...ikiwa ni pamoja na zengwe alizofanyiwa kipindi alichotaka kuwa Rais wa Daruso lakini Serikali na Chuo wakaogopa kwa kudhani kuwa UDSM patachafuka sana kwa migomo na dhambi zao zitatajwa kwa majina.................!!

Pia alikuwa mstari wa mbele katika kuongoza harakati mbalimbali pale mlimani zikiwepo harakati feki na zisizo feki...mfano halisi ni zile harakati za kuifuta 40% ambazo kiasi fulani tulifanikiwa na nyingine ndogondogo lakini kubwa zaidi ni hizi harakati feki za juzi ambazo aliziongoza yeye na ndugu zake kina OWAWA na SILINDE ambazo zilifanya vyuo vya umma vifungwe na wao wapate mabalaa na wengine kwenda kujificha mikoani.

Sitasahau jinsi tulivyimpigania kipindi alichofukuzwa chuo kwa hila kisa tu aligombea Urais na tukagoma mpaka akarudishwa yeye na wenzake na tukamuondoa rais mamluki bwana Pasience........!!

Kwanza namsifia kwa baadhi ya mambo aliyofanya he was a real HERO na kwa mambo mengine machache hayo sitaacha kumponda!!.Lakini intention ya huyu mganda ilikuwa ni nini?..bado ninajiuliza sana!!..na kwa nini alijiingiza katika vyama vya siasa vya nchini wakati yeye si raia??..bado najiuliza sana........!!

NENDA ODONG ODWAR TUTAKUKUMBUKA DAIMA....YOUR FOOTPRINTS ARE STILL THERE AT THE HILL!!

WASALIMIE MARAFIKI WA UGANDA....GOD BLESS YOU IN YOUR FUTURE ENDEVORS!!

Friday, December 5, 2008

IFMSO NA WANAFUNZI KAENI CHINI MJIULIZE??

Ninaamini kiongozi bora huonyesha dalili tangu akiwa kijana au mtoto kwa kuongoza vizuri jambo alilopewa au kutumia vizur madaraka aliyopewa.........!!
Hii inajumuisha viongozi mashuleni,vyuoni hata katika taasisi za dini....Mfano mzuri ni kwa Barrack Obama, mwana Afrika Mashariki na specifically Mjaluo aliyeshika ikulu yenye heshima zaidi dunian...alionyesha dalili hizo tangu akiwa shuleni...alipokuwa Harvard akisomea digrii ya sheria alikuwa kiongozi wa Association yao na bado alikuwa akijishughulisha na shughuli za Kijamii huko Chicago, Illinois!!

Lakini viongozi wa wanafunzi vyuoni mmeshindwa kuonyesha hilo na mmekuwa mkionyesha uzembe dhahiri katika maamuzi yenu na vtendo vyenu...inaonyesha kabisa hamfai kuwa viongozi wa taifa hili huko baadae!!

IFMSO au tunaweza kuwaita viongozi wa serikali ya wanafunzi IFM mmeonyesha uzembe mmkubwa wiki iliyopita kwa kuitisha wanafunzi wagomee ratiba ya mitihani iliyokuwa imebana!!waligoma siku mbili halafu mkawaambia watulie mnafanya mazungumzo na uongozi wa Chuo...................!!..........Kuonyesha uzembe zaidi nia kwamba baada ya hapo wiki iliyofuata wanafunzi walifanya mitihani kwa kufuata ratiba ileile waliyoigomea....hayo hayo kama wenzenu walioikataa sera na baadae wakaikubali!!

Sasa mliitisha mgomo wa nini??mlishindwa kufanya consultation na uongozi wabadili ratiba kabla ya kuitisha mgomo....au mliuandaa mgomo kwa maslahi binafsi??.......au mlikuwa mnataka muonyeshe kuwa IFM pia wanajua kugoma??
Viongozi viongozi acheni uzembe na badala yake mfanye vitu kisomi na sio kupotezea wanafunzi muda wao kwa sababu wanawaamini sana..........au mlikuwa mnataka mpate nafasi ya kusoma kwa sababu wiki ile mlikuwa mnajiandaa...!!

Msifanye nikakubaliana na walichosema kituo cha Clouds Fm kuwa mligomea mitihani sababu mlikuwa hamjajiandaa coz mnapenda sana starehe na wikend mnashinda sanaa pub.....!!

DON'T BITE ME WITH YOUR RESPONSE!!!!!!!!!!!!

WANAFUNZI NA VIONGOZI WA WANAFUNZI MMEKOSA MEDITATION!!


Saalam Wadau,

Ninaomba kulileta hili swala nikiwa na masikitiko makubwa sana.

Ninadhani wanafunzi wengi wengi waliingia kwenye migomo bila kufahamu ni nini impact ya migomo au bila kufahamu nini wanachodai au bila kufahamu kama maombi yao yatakubaliwa au lah....!!

Lakini vile vile nadhani walikuwa wamekosa meditation ya kujua ni njia nyingine ipi wanayoweza kutumia ili kufikisha madai yao!!

Ninasema hivyo kwa sababu mnamo leo asubuhi nilipita chuo kikuu cha Dar Es Salaam na kuona wanafunzi wengi sana wakiwa wamejazana internet cafe ya hall one kuchukua form za kuikubali sera ya kuchangia elimu ya juu ili warudi Chuoni...Sasa swali ni je kama waligomea sera hiyohiyo kwa nini sasa wanajaza form za kuikubali?? Je mlikuwa mnataka likizo fupi ya kukaa nyumbani au mlikuwa hamfahamu mnachodai??..mimi naona ya kwamba mmepungukiwa upeo na mmekosa meditation!!

Viongozi nyie ndio kabisa hamna kitu kwa sababu mliwekwa madarakani kusaidia wanafunzi,lakini sasa msaada wenu uko wapi endapo matatizo mliyotakiwa kuyashughulikia kisomi na kwa busara mnayaleta kwa wanafunzi wayashughulikie kwa njia ya migomo.......mmekosa meditation na nyie..hamfai kuitwa viongozi wa wanafunzi bali ni viongozi wa migomo.....nikiwa nimefocus moja kwa moja kwa DARUSO na wengine kwa sababu hamna mlichowasaidia wanafunzi mpaka sasa zaidi ya kuwa mmewaongezea matatizo na saivi mmekaa kimya!!

wanafunzi ada walizogomea ndio hiiiizo wanalipa ??sasa mmewasaidia nini wakati saivi wanahangaika mtaani kusaka ada ili warudi chuoni..........wengine siku walipofukuzwa chuo walilala vituo vya mabasi na watoto wa kike wakalala sehemu ambazo hazielezeki na za aibu na wengine wakaanza kutafuta nauli kwa njia zisizo nzuri.....

hamna mlichotusaidia wazembe nyie,.......................................!!..na wanafunzi msishabikie tu migomo bali muwe mnawaquestion viongozi ni steps zipi wamezifuata zikashindikana ndio sasa suluhisho ni mgomo!!...........

Mwisho nimeamini kuwa baadhi yenu mlitumiwa na vyama vya siasa kuendesha migomo na mlikuwa mnalipwa kwa kila siku ya mgomo.....!!


YOU BETTER CONTROL YOUR MINDS AND MEDITATE!!

MSAADA TUTANI!!

Bill,
Poleni kwa vyuo kufungwa.

Napenda kuomba msaada tutani kuhusu blog yangu. Mimi ni MAKULILO Jr, blog yangu
www.makulilo.blogspot.com nimeifanyia mabadiliko makubwa mno (SHUKRANI kwa Dada Subi, blogger www.nukta77.blogspot.com kwa 95% ya kuibadilisha blog hii, na kuiboresha zaidi). Napenda kuwaalika wadau wapate mambo mapya, mengi na muhimu kuhusu SCHOLARSHIPS, VOLUNTEERING, FREE TRAINING, INTERNSHIPS, FELLOWSHIPS, INTERNATIONAL JOBS etc. Pia website yangu www.makulilo.com ipo njiani kuja, wadau kaeni mkao wa kupokea michakato mingi mno nay a uhakika.

MDAU

MAKULILO Jr,
www.makulilo.blogspot.com
E-Mails: scholarships101@aol.com
Makulilo@marshall.edu
Cell phone +1 304 633 0978

Tuesday, December 2, 2008

NONDOOOZ ULAYA MAGHARIBI....

MA Human Rights Practice Scholarship

ERASMUS MUNDUS integrated masters degree programmes give students the opportunity to study at a variety of institutions across Europe. Scholarships are available to help fund postgraduate study for those coming to study from outside Europe.

Erasmus Mundus aims to improve the quality of higher education in Europe and to promote intercultural understanding with third countries. Erasmus Mundus supports high-quality masters programmes in Europe to promote the EU as an international centre of excellence in learning.
Programme length: two years, full-time
Programme start date: last week of August
Number of places: 35
Number of credits: 240
Award: The final degree is a joint award from Roehampton University, Göteborgs Universitet and Universitetet I Tromsø.
Locations:
Year one, Semester one: Göteborgs Universitet (Göteborg, Sweden)
Year two, Semester two: Roehampton University (London, UK)
Year two, Semester one: Universitetet I Tromsø (Tromsø, Norway)
Year two, Semester two: UK, Sweden or Norway for dissertation.
Scholarships
The EU Commission grants scholarships to highly qualified third-country graduate students and scholars. The grants are for students to follow a selected Erasmus Mundus master’s programme, and for scholars to carry out teaching and research assignments and scholarly work in the institutions participating in the programme. Students and scholars must apply to Roehampton University. The MA HRP consortia will apply to the EU Commission for scholarship funds. Scholarships are paid through the MA HRP consortia.‘Third-country student’ refers to a national of a country other than the EEA-EFTA states and candidate countries for accession to the EU, who:

has already obtained a first higher education degree
is not a resident of any of the member states
has not carried out his or her main activity for more than a total of 12 months over the last five years in any of the member states or the participating countries
has been accepted to register or is registered on an Erasmus Mundus master’s programme
Roehampton is involved in two collaborations:
MA Special Education Needs with Fontys University (Tilburg, The Netherlands) and Charles University (Prague, Czech Republic)
MA Human Rights Practice with Göteborgs Universitet (Göteborg, Sweden) and Universitetet I Tromsø (Tromsø, Norway)
Applications are currently being received for all students and scholars for entry in August. For those interested in applying for the Erasmus Mundus Scholarship the deadline is 14 December. For all other candidates (including European Students) the deadline is 30 June. Application formsApplication forms can be downloaded (below) or printed copies can be requested by emailing international@roehampton.ac.uk

Download student application form (Word doc)
Download scholar application form (Word doc)
Further information and application forms can be found on this website or requested from: Academic EnterpriseGrove HouseRoehampton UniversityLondonSW15 5PJ

Tel: +44 (0) 20 8392 3192
Fax: +44 (0) 20 8392 3031
Email: academic-enterprise@roehampton.ac.ukMoreinfo:
Click here SOURCE: http://cambodiajobs.blogspot.com/2008/12/ma-human-rights-practice-scholarship.html
FOR MORE OPPORTUNITIESVISIT http://www.makulilo.blogspot.com/
MDAU- MAKULILO Jr,
E-MAILS scholarships101@aol.commakulilo@marshall.edu