Tuesday, January 20, 2009

SIDHANI KAMA WATASOMA VIZURI....SINA UHAKIKA!!

Salamu Wadau
Samahani kwanza kwa kutoonekana kwa muda mrefu wala kutopata updates kwa muda mrefu!!
Ila ninafahmu wengi wenu mnaelewa kilichokuwa kinaedelea na hamtanilaumu kwani nilikuwa katika kipindi kigum mdau wenu,kipindi hicho kigumu kimesababishwa na viongozi wa chuo changu na wanaharakati feki kwa kuanzaisha migomo wasiyojua itatupeleka wapi.....kwani mpaka leo hii ninavyoongea mdauu wenu jina langu halijatoka na sijasajiliwa na masharti yote nimetimiza ila kwa mbinde.....!!

Nimepitia uzoefu flani mgumu katika maisha yangu ya elimu,uzoefu wa kugombana na chuo na serikali....na mwishowe nime concede defeat kwani chuo na serikali ndio vimepata ushindi na wenzetu wengi bado wako nyumbani hawajui hatma yao!!mungu wasaidie kwa sababu sio kosa lao kosa ni la siasa ilivyoingia vyuoni na viongozi wa wanafunzi wabovu na wanaharakati feki wasiotumia hoja na usomi bali nguvu!!wanafunzi wapatao 2000 inasemekana wamefutiwa udahili japo bado sijaaminiamini vile,na wengineo masikini wasioweza kulipa ada bado wako nyumbani....laana kwa viongozi mlioandaa mgomo na wanaharakati feki,na nyie chama cha siasa cha CHADEMA muwe makini siku nyingine mkiandaa mgomo,mmetupotezea marafiki wengi,vita vyenu na CCM pelekeni nje ya chuo!!vyama vyote vya siasa tawala na msio tawala tuko chini ya miguu yenu msitupotezee muda wetu wa masomo kama ni haki zetu tunazijua na tutaidai wenyewe hatutaki mikono yenu!!

Swali langu ni kwamba fujo zote zilizofanyika na masharti magumu yaliyowekwa na chuo..je wanafunzi watasoma vizuri kweli....maanayake wengi wako affected psycologically.........hata hao endapo chuo kitakuwa na huruma ya kuwarudisha sidhani kama watakuwa kawaida...mungu tusaidie!1Nakuja kwenu chuo kikuu cha Dar Es Salaam....Salamu kwako proffesor mkandala...baba naomba uwarudishe marafiki zetu chuoni,wengi sio kosa lao wanakuwa punished kwa kitu ambacho hawajafanya,kosa ni la wanaharakati feki na wachochezi ambao mimi siwaungi mkono na niko tayari hao wapoteze chuo na sio hao 2000 wasio na hatia,na nina mifano ya baadhi yao ambao hawakugoma kabisa...lakini inaonyesha hawatarudi chuoni...ninaomba uwasamehe mkuu!!
ninaongea haya kwa uchungu sana na ntaongea tena post ijayo!!

waliotimiza masharti ndio hivyo tayari wanarudishwa na wameshapewa vitambulisho vipya na karibia wanaanza masomo!!...mungu wangu wasaidie waliobaki ba wasaidie waanzae masomo vizuri ili wasiathirike na uzoefu mgumu waliopitia....!!...na ninaomba wanafunzi wabishi mpunguze ubishi wenu na tusolve matatizo yetu kisomi!!

Asanteni,Mdau Wenu
William!!

Monday, January 19, 2009

HII SIO ELIMU NI VITA........!!SOMA HAPA;

Viongozi wasisitiza wataandamana kushinikiza wenzao warejeshwe ::
Wapanga kuvaa vitambaa vyeusi kuomboleza msima elimu ya juu ::
Kamanda Kova aonya kama hawana kibali wasithubutu, watakiona cha moto
WANAFUNZI 2,000 wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam waliofutiwa udahili, wameapa kutumia kila mbinu kuhakikisha wanajiunga na wenzao chuoni hap oleo, wakitishia kuwa hata ikibidi wafe, basi wapo tayari. Moja ya mbinu walizopanga kuhakikisha wanafunguliwa lango kuu na kuingia chuoni, ni pamoja na kufanya maanadamano makubwa, yatayowalazimisha walinzi kufungua lango la kuingia chuoni.
Ingawa hawakuomba kibali cha polisi, wanafunzi hao wamesema watafanya maandamano hayo kwa amani, huku wakiwa wamevaa vitambaa vyeusi kuashiria msiba wa elimu ya juu Tanzania.

Mbali na maandamano hayo, baadhi ya viongozi wa wa wanafunzi wa chuo hicho kwa kushirikiana na wenzao kutoka Chuo Kikuu cha Sayansi ya Tiba na Afya cha Muhimbili (MUHAS), Umoja wa Vyuo vya Elimu ya Juu vya Umma Tanzania (UVEJUTA), wamesema wapo tayari kumwaga damu. “Kesho (leo) ni siku itakayotumika kumwaga damu za maskini ili kuleta haki katika elimu ya juu Tanzania. Bila haki hakuna amani,” alisema Rais wa Chama cha Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (DARUSO), Anthony Machibya, huku akiungwa mkono na viongozi wenzake ambao jana walikutana kupanga mikakati ya kufanikisha maandamano yao leo.

Aliwataka wanafunzi na wananchi walio jirani na chuo hicho kujitokeza kwa wingi kuwaunga mkono pale watakapoandamana kudai haki zao. Wakati wanafunzi hao wakijiandaa kwa maandamano hayo, Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limesema maandamano hayo ni batili na kuwataka viongozi hao wa wanafunzi wasijidanganye kufanya hivyo. “Sisi hatujiandai kwa ajili ya wanafunzi, sisi tuko tayari muda wote kuzuia uhalifu usitokee.

Kama wamesema wanaandamana wafanye hivyo kama wana kibali, vinginevyo watawajibika kwa kitakachotokea kwenye maandamano hayo,” alionya Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova. Kamanda Kova alisisitiza kuwa nchi lazima iendeshwe kwa kufuata sheria na kwamba hakuna mtu mwenye mamlaka ya kuamua anachotaka kufanya, hata kama kinapingana na sheria za nchi.

Kamanda Kova alisisitiza kuwaonya viongozi hao wa wanafunzi akisema kama hawana kibali, wasithubutu kuandamana kwani madhara ya kufanya hivyo wanayajua. Kutokana na matangazo ya chuo hicho, leo wananchi wa kawaida hawataruhusiwa kukanyaga ardhi ya Chuo Kikuu bila kuwa na kibali maalumu, ingawa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wataruhusiwa kuingia ili mradi tu wavae sare za shule zao. Hata hivyo, hadi jana mchana, mabasi yalikuwa yakiendelea kupitia katika eneo la Chuo Kikuu kama kawaida, tofauti na tangazo la chuo hicho lililotangaza kusitishwa kwa utaratibu wa kawaida wa usafiri hadi Januari 23, 2009.

Uongozi wa chuo hicho ulitangaza kuzifunga barabara zote zinazoingia katika chuo hicho ili kupisha usaili na udahili wa wanafunzi wanaorejea chuoni hapo kuanzia leo. Lango lililopo jirani na Chuo cha Maji lilitajwa kuwa litatumika kwa watu wanaoingia chuoni hapo tu na lile lililopo Chuo Kikuu cha Ardhi kuwa litatumiwa na wanaotoka. Wananchi watakaoathirika zaidi na zoezi hilo la siku tano ni wale wanaoishi maeneo hasa, Changanyikeni, Msewe na jeshini ambao njia zinazokwenda huko kupitia Chuo Kikuu zitafungwa. Godbless Charles, ambaye ni Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa MUHAS, alisema damu itakayomwagika ni ya wanyonge na ndiyo itakayotumika kuikomboa elimu ya juu ya kizazi kijacho. Charles ambaye pia ni Mwenyekiti wa UVEJUTA, alisema hawatanyamazishwa kwa milio ya bunduki, bali wataandamana kwa amani na kama ni vurugu zitaanzishwa na polisi walioandaliwa kuwazuia. Katibu wa Mtandao wa wanafunzi wa Vyuo Vikuu Tanzania (TSNP) ambaye pia ni Mbunge wa DARUSO, Owawa Stephen, aliwataka wanafunzi kuvaa nguo nyeusi au kufunga vitambaa vyeusi mikononi kuashiria msiba wa elimu ya juu nchini. “Hatutaingia chuoni kwa nguvu, tunachotaka ni haki yetu ya kudahiliwa, maandamano ni ya amani, wakitumia nguvu watupige tu, watawaua labda wawili na hata 10, lakini hatutasita kuidai haki yetu,” alisema huku akiungwa mkono na viongozi wenzake. Wakati wanafunzi hao wakiendelea na msimamo wao huo, menejimenti ya UDSM nayo imeendelea kushikilia msimamo wake wa kuwazuia wanafunzi walioshindwa kujaza fomu wasikanyage eneo la chuo ama sivyo hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.

Baadhi ya wakazi wanaoishi katika maeneo yanayozunguuka chuo hicho, ambao ili wafike ofisini kwao kwa urahisi, ni lazima wakanyage ardhi ya chuo, wameeleza kusikitishwa kwao na adhabu hiyo, ambayo walidai hawastahili. Jumaa Husein, mkazi wa Changanyikeni, alisema hali hiyo itawaathiri kwani watalazimika kuchelewa kazini kwa kuwa watalazimika kupita njia ndefu na mbovu. Madereva wa daladala zinazofanya safari zake Ubungo-Mwenge kupitia Chuo Kikuu, walisema hawajui wataishi vipi na familia zao katika kipindi cha siku hizo tano za kutopita chuoni hapo. Nacho Chama cha NCCR-Mageuzi kimeitaka Serikali kuchukua hatua za haraka kuhakikisha wanafunzi wote wanarejea chuoni na kuendelea na masomo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, Samuel Ruhuza, alisema Serikali imeshindwa kuweka wazi vipaumbele vya taifa katika kuboresha huduma muhimu za jamii. “NCCR-Mageuzi haichukulii kuwa wanafunzi waliotimiza masharti ya kulipa ada kama walivyoelekezwa kuwa ni kigezo cha kuamini kwamba wazazi waoa wana uwezo wa kulipia gharama za elimu ya juu. “Kwa sababu hii, tunaitaka Serikali iachane mara moja na utumiaji wa sera yake mbovu ya uchangiaji wa gharama za elimu ya juu na mikopo, wale wote wenye uwezo wa kufika Chuo Kikuu waweze kupata kile walichokikusudia,” alisema Ruhuza.

Tuesday, January 6, 2009

VYUOTZ IS LIKE NON-ALIGNED MOVEMENT!!

Heri ya mwaka mpya wadau,

Ninaamini wote mko vizuri na tuko tayari kwa ajili ya kuukabili mwaka 2009,ninawashukuru sana kwa kuonyesha sapoti yenu na kuendelea kutoa maoni mbalimbali ni vipi tuiendeshe blog yetu na ipate kuwajumuisha wanafunzi wote wa vyuo ndani na nje ya nchi bila kusahau wale alumni!!
Ningependa kutoa msimamo wetu kuhusu migomo kwani kuna watu katika maoni yao wamesema eti tunatetea upande wa fulani na watu fulani tunawaponda ambacho ni kitu kisicho sahihi.......!!
Post hizo chini tuliweka kwa kutambua athari wanazopata wasiouhusika pindi pande mbili hizo za serikali na viongozi wa wanafunzi wanapohitilafiana.....!!
Nikianza na makosa yanayofanywa na serikali....Kwanza Serikali haiwasikilizi viongozi wa wanafunzi pindi wanapotumia njia za kidiplomasia na kuonyeshwa dharau ya hali ya ju......Pili sera yao mbovu ya uchangiaji wa gharama za elimu ya juu ambazio zinawakandamiza masikini na kuwanufaisha matajiri,kwani huwezi kumpima mtu uwezo wake kwa kutumia makaratasi...Tatu Viongozi wa nchi kutowatembelea wanafunzi vyuoni na kujua matatizo yao na kuwasikiliza katika public talks wala kutobadilishana nao mawazo,wana assume vitu maofisini na kuja na maamuzi mabaya,hasahasa wanapaogopa UDSM mle Nkurumah hall.....Nne na si mwisho...Kutoshirikisha wadau wakuu ambao ni wanafunzi katika utunzi wa sera zinazowaathiri na kuwadanganya kuwa wamefanya utafiti ambao hau apply kwa mazingira ya TZ......!!
Ukija upande wa viongozi wa wanafunzi.....Kwanza Wengi wao hawawezi kutatua matatizo ya wanafunzi na badala yake huyaleta kwa wanafunzi wenyewe wayatatue kwa njia ya migomo.....Pili Wengine hufanya mambo ili kutafuta umaarufu na si kusaidia wanafunzi ili wa gain populatrity itakoyowasaidi kufulfill political interests zao hapo baadaye....Tatu Viongozi wengine wanatumiwa na vyama vya siasa kuchafua chama kingine ili ku fullfill interst za hivyo vyama!! Nne...Wengi wanaoongoza migomo si wale wanaofanya kweli zile kazi za kufuatilia utatuzi wa matatizo ya wanafunzi....yaani hawajawahi kufanya hizo diplomasia wala kufuatilia peacefull....wale ambao wanafuatilia unakuta wanashangaa tu migomo imekwishaanza!!
Hatupingi migomo ila athari zake ndio zinawaumiza wanafunzi ambao wanafukuzwa vyuoni na kurudi vijijini na vilevile kupoteza muda na kufanya vitu ambavyo havikutarajiwa...migomo ni mizuri pale unapofanya demonstration zisizo na athari kubwa kwa majority....si lazima tugoooome mpaka vyuo vifungwe hizo pande mbili zinafaidika lakini wanafunzi wengi innocent wanapata shida....!!
Hivyo kwa mwaka huu 2009 viongozi wa wanafunzi na serikali kuweni makini ili msisababishe athari kubwa kama zilizotokea mwaka 2008!!
Asanteni wadau na endeleeni kuisapoti blog kwa hali na mali!!

KWA WALE WATU WA SHERIA!!

United Nations International Law Fellowship Programme

The 2009 United Nations International Law Fellowship Programme will take place in the Peace Palace in The Hague/Netherlands from 6 July to 14 August 2009.
The 2009 Fellowship Programme will be conducted in English. Fluency in spoken and written English is required. The next Fellowship Programme in French will take place in 2010.
Candidates from the following countries, which were granted fellowships in 2008, are not eligible to apply for a fellowship in 2009:
Botswana, Brazil, China, Ecuador, the Gambia, Ghana, Iran (Islamic Republic of), Malawi, Mexico, Montenegro, Mozambique, Myanmar, Nepal, Saint Lucia and South Africa.
Application deadline: Wednesday, 25 February 2009
Course Content
The Programme comprises participation in seminars, attendance of lectures at

The Hague Academy of International Law,
as well as study visits.
Subjects on the course curriculum may include the following topics:
Law of Treaties, Intellectual Property Law, Law of the Sea, International Protection of Human Rights, Refugee Law, International Criminal Law, International Environmental Law, International Humanitarian Law, International Investment Law, Law of International Watercourses, International Trade Law, Recent Developments in International Law.
Financial Arrangements and Accommodation
The Programme will cover the fellowship recipient’s travel costs in economy class as well as medical insurance, the training material and the registration fee for The Hague Academy of International Law. In accordance with policies and procedures governing the administration of United Nations fellowships, participants will receive a stipend to cover their living expenses. Accommodation will also be provided by the Programme.
Additional places will be made available on a self-financed basis for participants who will have to take care of all the costs associated with their participation (travel, accommodation, living expenses, registration fee for The Hague Academy of International Law).

A more detailed description of previous courses can be viewed

here
.
For additional information, please consult our
"Frequently Asked Questions".
Application forms can be downloaded
here

SOURCE
http://www2.unitar.org/diplomacy/fell_internationallaw_E2.htm

For More Opportunities
MDAU-MAKULILO Jr,
www.makulilo.blogspot.com
+13046330978
E-mails
scholarships101@aol.com

makulilo@marshall.edu


SCHOLARSHIPS ZENYE DEADLINE ZA MAPEMA!!

Ndugu wadau,
Kwa ratiba za application kwa ajili ya mwaka wa masomo huu 2009 (mwezi August na September), ndio zinaelekea ukingoni. Hivyo, nimeweka list ya scholarships, hizi zote ni kutoka kwa ERASMUS MUNDUS
http://ec.europa.eu/education/programmes/mundus/projects/index_en.html. Kwa sheria za Mundus, huruhusiwi kufanya application zaidi ya tatu, hivyo chagua upendazo, na unazoona una sifa ndio ujaze, zikizidi tatu, inakula kwako.

Kama muonavyo, list hii kwa pembeni imeonesha DEADLINE yake, hivyo ni mwendo wa faster ktk kufanya application.

LIST
1. Environment
http://www.tu-harburg.de/eciu-gs/pro_joint_jemes.html Deadline 31st Jan 2009

2. Environment Science, Policy and Management
http://www.mespom.eu/node/26 Dedaline 9th Jan, 2009


3. Master in Informatics
http://www.eumi-school.org/edu/eumi/how_to_apply.xml?lang=en Deadline 18th Jan,2009

4. Space Master
http://www.spacemaster.se/index.php?option=com_content&task=view&id=14&Itemid=30 Deadline 15th Jan, 2009

5. Space Technology
http://www.aerospacemasters.org Deadline Febr 2, 2009


6. Security and Mobile Computing
http://www.tkk.fi/Units/CSE/NordSecMob/admission/index.html Deadline 9th Jan, 2009

7. Models and Methods of Quantative Economics
http://www.univ-paris1.fr/rubrique1297.html Deadline 6th Febr, 2009 Also at http://www.univ-paris1.fr/formation/eco_gestion/ufr27/study-in-english/erasmus_mundus/admissions_and_scholarships/article3971.html

8. Sustainable Forest and Nature Management
http://www.sufonama.net/eng/Home/home_7_26.html Deadline 16th Jan 2009
For More Opportunities,
MDAU- MAKULILO Jr,
www.makulilo.blogspot.com
+13046330978
E-mails
scholarships101@aol.com
makulilo@marshall.edu